• 2026-01-18 05:14
  • IT & Telecoms
  • Dar es Salaam
  • 42 views
Reference: 51
Job Details

Duties and Responsibilities

Kusimamia mifumo ya mawasiliano ya kidijitali ya Ofisi kama vile tovuti na mitandao ya kijamii;Kufanya ufuatiliaji na uchambuzi wa habari mbalimbali zinazohusu Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi;Kupiga na kuhariri picha mnato na picha mjongeo kwa ajili ya mawasiliano ya ndani na nje ya taasisi;Kuandaa picha na kubuni michoro yenye maudhui ya ukaguzi kwa ajili ya ripoti za ukaguzi, ripoti za wadau na maonesho;Kushiriki kampeni za mawasiliano ya kidijitali za Ofisi;Kutunza kanzidata ya ubunifu na kumbukumbu za mawasiliano; naKufanya kazi nyingine zinazoendana na fani yake kadri atakavyopangiwa na mkuu wake wa kazi.

QualificationsKuajiriwa wenye Shahada ya kwanza katika fani ya “Multimedia Technology” (Bachelor of Science in Multimedia Technology) au Shahada ya Sanaa katika Ubunifu wa Michoro (Bachelor of Arts in Graphic Design kutoka katika Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

RemunerationTGS D

Company Description
Historia ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Kabla na Baada ya UhuruHistoria ya Ofisi hii inahusiana kwa karibu na historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baada ya Mkutano wa Berlin wa mwaka 1885, sehemu ya ardhi ambayo kwa sasa ni Tanzania Bara iligawiwa kwa Wajerumani. Mwaka 1897, eneo hili liliitwa Himaya ya Ujerumani ya Afrika Mashariki na lilikuwa koloni la Ujerumani mpaka mwaka 1919. Baada ya Vita vya Kwanza vya Dunia, kupitia Mkataba wa Versailles, Waingereza walipewa haki ya kulitawala eneo hili, ambalo wakati huo lilianza kuitwa Tanganyika. Baada ya Vita vya Pili vya Dunia mwaka 1946, Tanganyika iliwekwa chini ya Mamlaka ya Umoja wa Mataifa chini ya uangalizi wa Uingereza.Desemba 1961, Tanganyika ilipata uhuru wake kutoka kwa Waingereza na kuendelea kuwa sehemu ya Jumuiya ya Madola. Mwaka 1962, Tanganyika ikawa Jamhuri. Tanganyika iliungana na Zanzibar tarehe 26 Aprili 1964 na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Summary