• 2026-01-17 23:09
  • Public Service
  • Dar es Salaam
  • 18 views
Reference: 27
Job Details

Duties and ResponsibilitiesKushiriki katika kuainisha maeneo ya ukaguzi na kutunza kumbukumbu zake;Kushiriki katika kuandaa mipango kazi ya ukaguzi;Kukusanya na kutunza taarifa kwa ajili ya kufanya ukaguzi;Kushiriki katika kufanya na kutayarisha taarifa za upembuzi yakinifu, mipango kazi na randama ya tafiti za awali;Kushiriki katika uchanganuzi wa taarifa na kuandaa rasimu za taarifa za ukaguzi;Kuainisha maeneo yanayoweza kukaguliwa na kutunza taarifa za ukaguzi; naKufanya kazi nyingine zinazoendana na fani yake kadri atakavyopangiwa na mkuu wake wa kazi.

QualificationsKuajiriwa wenye Shahada ya Kwanza ya Uhandisi wa Umeme ( Bachelor of Electrical Engineering) kutoka katika Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali waliosajiliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB).

RemunerationSAIS. E

Company Description
Historia ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Kabla na Baada ya UhuruHistoria ya Ofisi hii inahusiana kwa karibu na historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baada ya Mkutano wa Berlin wa mwaka 1885, sehemu ya ardhi ambayo kwa sasa ni Tanzania Bara iligawiwa kwa Wajerumani. Mwaka 1897, eneo hili liliitwa Himaya ya Ujerumani ya Afrika Mashariki na lilikuwa koloni la Ujerumani mpaka mwaka 1919. Baada ya Vita vya Kwanza vya Dunia, kupitia Mkataba wa Versailles, Waingereza walipewa haki ya kulitawala eneo hili, ambalo wakati huo lilianza kuitwa Tanganyika. Baada ya Vita vya Pili vya Dunia mwaka 1946, Tanganyika iliwekwa chini ya Mamlaka ya Umoja wa Mataifa chini ya uangalizi wa Uingereza.Desemba 1961, Tanganyika ilipata uhuru wake kutoka kwa Waingereza na kuendelea kuwa sehemu ya Jumuiya ya Madola. Mwaka 1962, Tanganyika ikawa Jamhuri. Tanganyika iliungana na Zanzibar tarehe 26 Aprili 1964 na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Summary